TACATDP
Maelezo
Hii ni programu mahsusi ya benki ya CRDB yenye kutoa mikopo ya riba nafuu, mafunzo, bima na udhamini kwa wakulima wa Tanzania, inayofadhiliwa na mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kusaidia nchi kutatua changamoto au athari za mabadiliko ya tabia nchi (Green Climate Fund) kwenye sekta ya kilimo kwa mazao ya chakula.
Hii ni programu mahsusi ya benki ya CRDB yenye kutoa mikopo ya riba nafuu, mafunzo, bima na udhamini kwa wakulima wa Tanzania, inayofadhiliwa na mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kusaidia nchi kutatua changamoto au athari za mabadiliko ya tabia nchi (Green Climate Fund) kwenye sekta ya kilimo kwa mazao ya chakula.
• Kununua au kujenga ghala la kuhifadhi chakula lililojengwa kwa tofali za udongo zilizokaushwa kwa jua, chuma au bati.
• Teknolojia na mbinu za kuepusha upotevu wa mazao na chakula.
• Kununua au kujenga nyumba kitalu (Green House).
• Kujenga bwawa au kuchimba kisima cha maji au kuvuna maji ya mvua kwa ajili ya kumwagilia shambani.
• Kununua na kufunga pampu ya umwagiliaji ya kutumia nishati ya umeme jua (solar).
• Kilimo cha umwagiliaji wa matone au mitaro iliyoboreshwa
• Kulima mazao mchanganyiko au kilimo mseto.
• Kulima mazao mzunguko.
• Kilimo cha matuta kupunguza kasi ya maji kwenye miiinuko au miteremko.
• Kununua au kuzalisha mbolea ya asili (samadi, mabaki ya mimea, mabaki ya mazao, taka za vyakula n.k).
• Kununua mbegu bora inayostahimili ukame iliyopendekezwa na wataalam.
• Kulima kilimo kisichotumia udongo (hydroponics)
• Kulima mazao au miti kinga upepo shambani
• Teknolojia na mbinu za kuongeza unyevu kwenye udongo
Mikopo hii ya CRDB inatolewa ili kuongeza uhimilivu wa athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa wakulima wa mazao ya chakula ili kuwawezesha kumudu teknolojia au kununua zana/nyenzo bora za kilimo hasa za asili na zenye kulinda mazingira na kutunza rutuba ya udongo.
Mkulima yeyote (mmoja mmoja, kikundi, AMCOS, SACCOS), wa kati, mkubwa) kama anahitaji kununua au kutumia mbinu bora zenye kuongeza ufanisi na mavuno shambani kwake anaweza kuomba mkopo huu. Vigezo na masharti ya mikopo ya benki ya CRDB vitazingatiwa.
Mikopo wa mtaji wa muda mfupi ambao utalipwa baada ya mavuno
• Mikopo ya muda wa kati
• Mikipo ya muda mrefu
Tembelea tawi la Benki ya CRDB au Wakala
Tupigie Bure: 0800 008 000 au +255 755 197 700
au tuandikie barua pepe: [email protected]
Unaweza kupendezwa na
Mkopo wa SME Bidii
Hii ni bidhaa iliyobuniwa kumuwezesha mfanyabiasha mdogo na mfanyabiashara wa kati kuweza kukidhi mahitaji yao ya mtaji wa uwekezaji.
Mkopo wa Malkia
Pendekezo la CRDB Malkia ni kifurushi cha bidhaa na huduma zilizopo za benki zilizounganishwa pamoja na kulengwa katika kuimarisha ufikiaji wa wanawake wa huduma za kifedha na zisizo za kifedha.
MSE Loans
These are small ticket facilities issued to formal and informal micro and small enterprises with target to grow and expand small and sustainable business.
Mkopo wa Komboa
Komboa mizigo yako iliyokwama bandarini na uendelee na biashara yako kupitia Mkopo wa CRDB Bank Komboa.
MSE Asset Financing
Is a financing solution extended to MSE customers to finance acquisition of business vehicles.
Overdraft Facilities
The Overdraft Facility gives entrepreneurs financial flexibility to allow businesses to meet working capital needs.
Local Purchase Order Finance
Short-term transaction-based loan used to improve customer’s business
Invoice Discounting Finance
IDF allows SME businesses to borrow funds against confirmed unpaid invoices
Certificate Discounting Finance
CDF allows SME customers to borrow funds against unpaid Certificates
SME Asset Financing
Is a financing solution extended to customers to finance investments in specific assets.
Investment Financing
These are loans for acquisition of items that are used for investment purposes
Mkopo wa Green Bond
Mkopo kwa miradi inayozingatia utunzaji wa Mazingira